Loading...

WAWILI WAFA PAPO HAPO NA WATATU WAJERUHIWA VIBAYA

Na Gideon Mwakanosya, Songea
 
WATU  wawili wamefariki dunia na wengine watatu akiwemo dereva wa gari hilo wamejeruhiwa vibaya mkoani Ruvuma baada ya kugongwa na gari katika  eneo la Mahenge katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea baadaya ya kugongwa na gari la Jeshi la wananchi (JWTZ)  la Makao makuu ya brigedi Chandamali
 
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Michael  kamuhanda amesema kuwa tukio hilo limetokea  majira ya saaa mbili na nusu asubuhi huko kwenye barabara ya Songea na Namtumbo ambapo aliwataja waliokufa kuwa ni Stumai Moyo (20) na Tabia Bilali (23) wote wakazi wa eneo la Mahenge wa Songea mjini na walio jeruhiwa vibaya ni Amina Moyo (2) na Issa Moyo (65) wote wakazi wa Mahenge ambao baada ya kutokea ajali hiyo walikimbizwa katika Hospitali ya mkoa ambako wamelazwa 
 
 Alifafanua zaidi  kuwa gari hiyo Landlover Discova yenye namba za usajili 1513 JW 97  iliyosababisha ajali na kuuwa watu wawili papohapo na wengine wawili kujeruhiwa vibaya.
 
Alieleza zaidi kuwa gari hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na  MT 97812 SGT Kelvin Muhagama ilikuwa ikitoka Makao makuu ya Brigedi Chandamali na kuelekea Songea mjini  
 
Kamanda Kamuhanda alibainisha zaidi kuwa chanzo cha ajari hiyo ni mwendo kasi ambao ilimsababisha dereva wa gari hilo kushindwa kumudu usukani
 
Naye Mganga mfawidhi wa Hospitali ya mkoa songea  Dr. Mathayo Chanangula amethibitisha kupokea maiti za watu wawili ambazo kwa sasa zimehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali hiyo  na majeruhi  watatu ambao wawili kati yao wamelazwa kwenye wodi za majeruhi na majeruhi mmoja ambaye ni mtoto wa umri wa mika 2 Amina Moyo amekimbizwa katika Hospitali ya Mision ya Peramiho kwa matibabu zaidi baada ya Hospitali hiyo kukosa mashine ya Ex –ray kwani imeonekana kuwa Amina ameumia kichwani ambako kunahitaji kupata vipimo vya Ex –ray ambapo kwa sasa hivi huduma hiyo inapatikana katika Hospitali ya Mision ya Peramiho
 
Dr. Chanangula alifafanua zaidi kuwa kwa muda mrefu hospitali ya mkoa songea haina kabisa huduma ya Ex –ray tangu mashine hiyo ilipo haribika na kwamba kwa hivi sasa wanasubiri mafundi kutoka ufiripino waje kitengeneza jambo ambalo limeonekana kuwa kero kuwa kwa wakazi wa songea ambao wamefika kupatiwa huduma hiyo lakini wamekuwa wakielekezwa kwenda Hospitali ya Mision ya Peramiho ambayo iko umbali wa kilometa 25 toka Songea mjini



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top