Loading...

DIWANI WA CHADEMA ATAKA UFAFANUZI JUU YA MATUMIZI YA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO SONGEA MJINI

DIWANI wa kata ya mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA)katika  Halmashauri ya manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Joseph Fuime amemtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo kutoa ufafanuzi  ambao unatumika kuchukuwa fedha za mfuko wa Jimbo na zinatumika katika matumizi gani na wanafunzi wanaosaidiwa kupitia mfuko huo ni wenye sifa zipi.


Hayo aliyasema jana wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ambapo alitaka kujuwa maelezo ya wanafunzi 150 ambao wanasomeshwa na mfuko wa Jimbo  baadhi yao kuto ripoti mashuleni kwa kigezo cha kutolipiwa ada.

“Mwenyekiti naomba mkurugenzi alieleze baraza hili juu ya mtiririko upi wa fedha za mfuko wa jimbo zinaletwa ,utaratibu gani unatumika katika kuzileta hizo fedha na zikija zinaenda wapi maana kwenye makabrasha yenu mmeandika kuwa zinalipia ada wanafunzi 123 wakati baadhi yao wapo tu majumbani kwa sababu ya kukosa ada naomba majibu.”alisema  Fuime.


Kwa upande wake meya  wa manispaa hiyo Charles Muhagama alisema kuwa fedha za mfuko wa jimbo haziji kwa mtiririko wa aina yoyote ile isipokuwa zinaletwa kwa aajiri ya maendeleo ya jimbo hata hivyo fedha hizo huwa zinachelewa kuletwa lakini watoto hawajazuiwa kuripoti mashuleni.


Alifafanua zaidi kuwa zaidi ya watoto 150 wanasomeshwa na mfuko huo waliopo kwenye mazingira magumu na kwamba fedha za mfuko wa jimbo kwa mara ya mwisho zimeingia juni mwaka jana na kati ya watoto hao 123 wanasoma sekondari,watoto wan ne wanasoma vyuo vikuu na 23 wanasoma vyuo mbalimbali.


Hata hivyo amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Songea mjini Dr. Emanuel Nchimbi ambaye pia ni Waziri wa mambo ya Ndani kwa moyo wake wa kuyelekeza fedha hizo zisomeshee watoto wasio na uwezo na wanaoishi katika mazingira magumu kwani angeweza kuelekeza fedha hizo kwenye miradi mingine ya maendeleo lakini kwa kutambua umuhimu wa elimu ameamua kuelekeza nguvu zake kwenye elimu.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top