Loading...

Waasi wa Seleka wateka mji muhimu, CAR


Waasi wa Seleka wauteka mji muhimu kusini mwa CAR
Kundi moja la waasi katika Jamhuri ya Afrika ya kati CAR, limeuteka mji muhimu kusini mashariki mwa nchi hiyo karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Duru zimearifu kuwa Jeshi lilijiondoa kutoka mji wa Bangassou bila pingamizi yoyote. Kundi hilo la Seleka lilisaini mkataba na serikali mwanzoni mwa mwaka huu na likapewa uongozi wa baadhi ya wizara kuu za serikali. Hata hivyo tangu wakati huo limekuwa likilalamikia baadhi ya masuala linalodai kuwa hayajatatuliwa.

Seleka ni nani?

Seleka (jina hilo likimaanisha muunguano) liliteka miji mingi nchini humo na hata kutishia kuuteka mji mkuu Bangui. Walisaini mkataba na serikali mnamo Januari 11 katika mji mkuu wa Gabon Libreville chini ya utawala wa Francoise Bezize.
Mkataba huo ulifanikishwa kwa upatanishi wa viongozi wa eneo hilo na uliunda serikali ya muungano wa kitaifa na sasa inaongozwa na kiongozi wa upinzani Nicolas Tiangaye.
Tangu kuundwa serikali hiyo Seleka wamekuwa wakitilia shaka nia ya serikali na kuilaumu kwa kuendesha serikali mbadala inayohujumu nafasi yao. Wametishia kujiondoa kutoka serikalini mara kadhaa.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top