Loading...

ZOEZI LA UCHAGUZI WA PAPA MPYA WA KANISA KATOLIKI DUNIANI:

ZOEZI LA UCHAGUZI WA PAPA MPYA WA KANISA KATOLIKI DUNIANI:

Zoezi lilianza jana kwa makadinali kutoka duniani kote kukusanyika huko St. Peters Square kwa ajili ya kuchagua papa mpya atakayeliongoza kanisa katoliki duniani. Hii ni kufuatia kujiuzulu kwa Papa Benedict XVI kutokana na umri mkubwa.

Zoezi hilo halijafanikiwa katika raundi ya kwanza baada ya moshi mweusi kuonekana jana. Hiyo ni ishara ya kutopata papa mpya na mchakato unaendelea.

Mchakato wa kuchagua Papa mpya huanza kwa kukusanyika kwa makadinali 115 wenye umri wa chini ya miaka 80 kutoka duniani kote. Makadinali hujifungia ndani bila mawasiliano yeyote na dunia, mpaka pale Papa atakapopatikana. Baada ya sala na maombi, makadinali hao kila mmoja hutakiwa kupendekeza jina moja la Kadinali ambaye wanadhani anafaa kuwa Papa. 

Ushindi wa Kadinali kuwa Papa unategemea zaidi ya 2/3 ya mapendekezo yote, kwa maana hii, Kadinali anatakiwa kupata zaidi ya mapendekezo 77 ili awe Papa. 

Mchakato usipofanikiwa, karatasi hizo za mapendekezo huchomwa kwa kemikali maalum ambazo husababisha moshi mweusi, ishara kwa dunia ya kwamba bado Papa mpya hajapatikana. Mchakato utaendelea mpaka pale dunia itakaposhuhudia moshi mweupe. Hiyo ni ishara kwamba Papa mpya amekwisha patikana, na dunia ipo tayari kumsikia.

Tunawatakia kila la kheri Kanisa Katoliki katika uchaguzi wa Papa mpya.

Zoezi lilianza jana kwa makadinali kutoka duniani kote kukusanyika huko St. Peters Square kwa ajili ya kuchagua papa mpya atakayeliongoza kanisa katoliki duniani. Hii ni kufuatia kujiuzulu kwa Papa Benedict XVI kutokana na umri mkubwa.

Zoezi hilo halijafanikiwa katika raundi ya kwanza baada ya moshi mweusi kuonekana jana. Hiyo ni ishara ya kutopata papa mpya na mchakato unaendelea.

Mchakato wa kuchagua Papa mpya huanza kwa kukusanyika kwa makadinali 115 wenye umri wa chini ya miaka 80 kutoka duniani kote. Makadinali hujifungia ndani bila mawasiliano yeyote na dunia, mpaka pale Papa atakapopatikana. Baada ya sala na maombi, makadinali hao kila mmoja hutakiwa kupendekeza jina moja la Kadinali ambaye wanadhani anafaa kuwa Papa.

Ushindi wa Kadinali kuwa Papa unategemea zaidi ya 2/3 ya mapendekezo yote, kwa maana hii, Kadinali anatakiwa kupata zaidi ya mapendekezo 77 ili awe Papa.

Mchakato usipofanikiwa, karatasi hizo za mapendekezo huchomwa kwa kemikali maalum ambazo husababisha moshi mweusi, ishara kwa dunia ya kwamba bado Papa mpya hajapatikana. Mchakato utaendelea mpaka pale dunia itakaposhuhudia moshi mweupe. Hiyo ni ishara kwamba Papa mpya amekwisha patikana, na dunia ipo tayari kumsikia.

Tunawatakia kila la kheri Kanisa Katoliki katika uchaguzi wa Papa mpya.

Like · ·


Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top