Loading...

Kamati ya Mauaji Mkoa wa Ruvuma Yatoa Taarifa


KAMATI iliyoundwa na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu kuchunguza chanzo cha mauaji ya watu waliouwawa kuhusiana na imani za kishirikina na kusababisha vurugu za watu kuandamana na iliyopolekea mauaji ya watu wawili imekamilika.

Kamati hiyo iliyoundwa na watu wanane ikiongozwa na katibu tawala msaidizi miundombinu Severin Tossi ili Serikali iweze kuchukuwa hatua na kuhakikisha mambo kama hayo hayatokei tena

Akitoa taarifa hiyo Mwambungu alisema kuwa wale wote waliotuhumiwa kwenye mauaji hayo wamefikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Hata hivyo alisema kuwa kamati hiyo imeshindwa kuthibitisha uvumi wa watu kumi na nne waliouwawa kwa kuhusishwa na imani za kishirikina na kwamba tabia ya watu kueneza uvumi wa uongo ni mbaya sana kwani inagharama kubwa kwa wananchi na kuongeza kuwa kamati hiyo imefatilia na kupata taarifa kuwa hakuna mtu yoyote aliyenyofolewa viungo vya siri .

“Naomba nitoe rai kwenu kuwa tabia hii ya uenezaji wa uvumi ni mbaya sana kwa sababu inagharama kubwa sana kwa wananchi ambao wanashindwa kufanya kazi zao za kila siku katika ujenzi wa Taifa.”alisema Mwambungu.

Amesema,tayari elimu kwa wananchi imeshatolewa na wananchi wameanza kufanya kazi ya ulinzi shirikishi kwa kushirikiana na polisi kata ambapo kazi ya ulinzi na kwamba mitaa yote ya Manispaa ulinzi umeimalishwa.

Mwambungu ameongeza kuwa, kwa sasa hali ya utulivu na usalama katika mkoa wa Ruvuma imerejea kama awali ambapo wananchi wanaendelea na shughuli zao za kila siku kama kawaida .

“Napenda kuwahakikishia wananchi wa mkoa wa Ruvuma na watu wanaoishi nje ya mkoa wa Ruvuma kuwa Songea ni salama na wananchi wanaendelea na shuguli zao kama kawaida, nawashukuru wananchi kwa ushirikiano mkubwa ambao wameutoa pia wanahabari kwa kusaidia kurejesha hali ya utulivu na amani ”alisema

Aidha, amewataka wananchi kuelewewa umuhimu wa kujilinda na kufata sheria ikiwa ni pamoja na kuacha hulka ya kujichukulia hatua mkononi ,ikiwa ni pamoja na kuacha kujihusisha na tabia za uvumi na hisia za kishirikina ili kuimarisha amani na utulivu.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top