Loading...

WANAFUNZI WA KIKE WA SHULE YA SEKONDARI DE PAUL WAKUMBWA NA UGONJWA WA AJABU



BAADHI ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya De Paul inayomilikwa na kanisa la katoliki jimbo kuu la Mbinga mkoani Ruvuma wamekumbwa na ugonjwa unaodaiwa kuwa ni wa ajabu ambao umekuwa ukiwasababibishia kuweweseka na baadhi ya viungo vya miili yao kupooza.

Habari zilizopatikana kutoka kwenye shule hiyo ambayo ipo umbali wa kilometa 15 kutoka Mbinga mjini zimesema kuwa siku tatu zilizopita dalili zilianza kuonekana kwa baadhi ya wanafunzi ambao baadae hali zao ziliendelea kuwa mbaya na uongozi wa shule ulilazimika kuwakimbiza kwenye hospitali ya wilaya ya Mbinga kwa ajili ya kupata matibabu ambapo wanafunzi tisa kwa mara ya kwanza walikumbwa na ugonjwa huo wa kuweweseka na kupooza baadhi ya viungo vya miili yao.

Habari zaidi ambazo zimeelezwa na baadhi ya wanafunzi na walimu ambao wameomba majina yao yahifadhiwe zilisema kuwa siku ya pili wanafunzi wengine saba walibainika kuwa na tatizo hilo nao walipelekwa katika hospitali ya serikali ya wilaya kwa matibabu ambako kati yao walilazwa na wengine waliruhisiwa kurudi kwa nyumbani kwa wazazi wao.

Hata hivyo jitihada za kuupata uongozi wa shule hiyo ziligonga mwamba baada ya kutopatikana kwa simu zao za mikononi ambapo jitihada zilifanywa za kumpata mganga mkuu wa wilaya ya Mbinga Dr. Damas Kayela ambaye alikiri kuwapokea wanafunzi kumi na sita ambao waliletwa wakiwa wanaumwa kwenye hospitali ya wilaya hiyo.

Dr. Kayela alifafanua zaidi kuwa baada ya kuwapokea wagonjwa hao jopo la madaktari lilianza kuwahudumia kwa kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na matatizo yaliyokuwa yanawakabiri lakini baadae jopo la madaktari lililazimika kwenda kwenye eneo la shule ya De Paul ambapo walipofika waliwakuta wanafunzi wengine sita wakiwa wanasumbuliwa na tatizo hilo kasha walitoa huduma kwa kuwasaidia na baadaye iligundulika kuwa tatizo lililowakumba wanafunzi hao ni la ugonjwa wa kuchanganyikiwa na kulegea mwili.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga alipohojiwa kuhusiana na tatizo hilo lililotokea kwenye shule ya sekondari ya De Paul ambayo ipo katika kijiji cha Mbangamawe alithibitisha kuwa wanafunzi ishirini na mbili wa shule hiyo waligungulika kuwa na ugonjwa wa kuchanganyikiwa na kulegea mwili na kwamba kwa sasa hivi wataalamu wa afya wakiwemo madaktari walishakwenda kwenye shule hiyo kutoa ushauri zaidi kwa wanafunzi na uongozi wa shule hiyo.

Ngaga alifafanua zaidi kuwa tatizo la wanafunzi kukumbwa na ugonjwa huo tayari ofisi yake imeshaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa linakwisha na vile vile ameiagiza timu hiyo ya wataalamu kufanya utafiti zaidi na ikiwezekana hata kwa shule zingine za sekondari za wilaya hiyo ziepukane na kukumbwa na ugonjwa huo ambao unawanyemelea zaidi wanfunzi wa kike.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top