Loading...

RC MWAMBUNGU-ATOA SIKU 14 KWA WAZAZI WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUINGIA KIDATO CHA KWANZA AMBAO BADO HAWAJARIPOTI KWENYE SHULE WALIZOPANGIWA

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu  ametoa siku 14 kwa wazazi wenye  watoto waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza Januari mwaka huu katika shule za sekondari ambao mpaka sasa hawajaripoti  kwenye shule walizopangiwa na wahakikishe kuwa wanawapeleka shuleni watoto hao haraka iwezekanavyo.

Mwambungu amelitoa agizo hilo jana mchana ofisini kwake wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara aliyoifanya kwenye baadhi ya shule za sekondari kila Wilaya mkoani humo ambako amegunduwa kuwa nusu ya wanafunzi waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza mkoani humo mpaka jana hawajaripoti kwenye shule walizopangiwa.

Alisema kuwa  jumla ya wanafunzi 16,578 walichaguliwa kuanza masomo ya sekondari Januari mwaka huu lakini kati ya hao walioripoti ambao hivi sasa wanaendelea na masomo 9,388 na wanafunzi 7190 ambayo sawa na asilimia 56.6 hawajaripoti kwenye shule walizopangiwa.

Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa katika ziara ya kushtukiza aliyoifanya kwenye baadhi ya shule amegunduwa kuwa idadi ndogo ya wananfunzi ambao wapo madarasani wanaendelea na masomo na wanafunzi wengine hawajulikani wapo wapi jambo amblo limepelekea kuwepo na hofu kubwa kwa wazazi wa wenye watoto kutoona umuhimu wa kuwapeleka watoto wao shuleni.

Alitoa mfano wanafunzi wa kidato cha kwanza waliochaguliwa na kujiunga na masomo ya sekondari mwaka katika shule ya Sekondari ya Barabarani iliyopo Wilaya ya Songea vijijini ambapo wanafunzi 20 walipangwa kuripoti lakini hadi jana ni wanafunzi wawili tu ambao wameripoti shuleni hapo hali ambayo imemtisha mkuu huyo wa Mkoa.

Amezitaja shule zingine za sekondari ambazo wanafunzi hawajaripoti kwa kiwango kinachostahili ni pamoja na sekondari ya serikali ya  kutwa ya Mtutura iliyopo wilayani Tunduru kuwa walipangwa wanafunzi 159 kati ya hao walioripoti ni wanafunzi 22 na kwamba 137 hawajaripoti na hawajulikani walipo.

Alisema kuwa kutokana na hali hiyo iliyojitokeza amewaagiza wakuu wa Wilaya pamoja na wakurugenzi wa halmashauri za Wilaya na Manispaa,wenye viti wa halmashauri pamoja na maafisa elimu wa sekondari wahakikishe kuwa wanafuatilia kwa karibu wazazi wa watoto waliochaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari mwaka huu na amewataka Hadi ifikapo Machi moja mwaka huu wawe wameshafika kuripoti kwenye shule walizopangiwa na kuanza masomo mara moja.

Amewaonya wakuu wa shule za sekondari za serikali kuacha mara moja tabia ya kuwarudisha watoto nyumbani kwa madai kuwa wameshindwa kulipa ada na michango na kwamba watakao bainika watachukuliwa hatua mara moja na si vinginevyo pia wazazi wa wanafunzi ambao watoto wao watashindwa kuripoti kwenye shule walizopangiwa watakamatwa na kufikishwa mahakamani mara moja .

Hata hivyo Mwambungu amewaonya baadhi ya watu wenye tabia chafu ya kufanya mapenzi na wanafunzi wa kike na kuwasababishia washindwe kuendelea na masomo kwa mfano shule ya sekondari Nasuri iliyopo wilayani Namtumbo wanafunzi 14 wamekatishwa masomo kutokana na kupata ujauzito pamoja na shule ya sekondari ya serekali ya kutwa ya Lukara iliyopo Songea vijijini wanafunzi 12 wamebainika kuwa ni wajawazito.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top