Loading...

MBUNGE JENISTA AMWAGA VITANDA ZAHANATI YA NAMBENDO

MBUNGE wa Jimbo la Peramiho Wilaya ya Songea vijijini mkoani Ruvuma Jenista Mhagama ametoa msaada wa vitanda sita na magodoro sita wenye thamani ya sh.milioni 1.7 kwaajiri ya akina mama wajawazito katika zahanati ya kijiji cha Nambendo ambacho kiko mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi ya mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Songea Diwani wa kata ya Ndingosi Visenti Komba alisema kuwa mbunge wa jimbo hilo ametekeleza ahadi yake aliyokuwa ameitoa kwa wananchi wa kijiji hicho wakati alipokuwa amewatembelea ambako aliahidi kuhakikisha kuwa anawasaidia akina mama wajawazito.
 
Alisema kuwa Mbunge huyo ametoa msaada wa vitanda sita vyenye thamani ya sh. milioni   1.5 pamoja na magodoro sita yenye thamani ya sh.210,000 na kwamba msaada huo umewafurahisha kwa kiasi kikubwa wakina mama wajawazito ambao wamekuwa wakienda kusubiri kujifungua kwenye zahanati hiyo ambayo hapo awali ilikuwa na vitanda viwili tu.
 
Diwani Komba alieleza kuwa pamoja na kupokea msaada huo kutoka kwa mbunge bado zahanati hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa madawa pamoja na vifaa tiba na vitendea kazi jambo ambalo linawalazimu kutembea umbali wa kilomita 43 kwenda kupata huduma hiyo katika kijiji cha ndongosi ambako kuna zahanati inayomilikiwa na kanisa katoliki jimbo kuu la Songea.
 
Alieleza kuwa tayari wananchi wa kijiji hicho walishajenga wodi mbili kwaajiri ya kujitazamia akina mama wajawazito wakati wanatarajia kujifungua hivyo wanaiomba serikali kupitia fedha za wafadhili (busket fund) kuelekeza kwenye ujenzi wa wodi hizo ili ziweze kuboresha zaidi miundo mbinu ya zahanati hiyo.
 
Hata hivyo Diwani wa kata hiyo Komba amemshukuru mbunge Jenista kwa msaada mkubwa alioutoa kwa wananchi wa kijiji cha Nambendo ambacho kipo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji na kipo mbali na kituo cha afya cha Muhukuru.
 
Kwa Upande wake wananchi wa kijiji hicho wamempongeza mbunge Jenista kwa kuona umuhimu wa kuwaletea vitanda pamoja na magodoro kwani wanawake wengi wamepoteza maisha kutokana na kukosekana kwa vifaa tiba na vitendea kazi katika zahanati hiyo.
 



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top