Loading...

TANESCO SONGEA YATANGAZA MGAO WA UMEME

MTAMBO mmoja wa kufulia umeme kati ya mitambo mitambo ya shirika la umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Ruvuma umedaiwa kuwa na itilafu na kusababisha kuwepo na mgao mklai wa umeme katika halmashauri ya manispaa ya Songea na vitongoji vyake.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ukumbi wa mikutano wa maliasili wa ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Meneja wa Tanesco mkoani humo Mhandisi Monika Kebara alisema kuwa mtambo ambao umeharibika ni ule aliokuwa ameuleta raisi wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete katika ahadi zake alizoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka juzi mjini Songea.
Alisema kuwa mtambo huo wa kufulia umeme wa megawati 1.9 ulianza kukorofisha toka wiki iliyopita hivyo kusababisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa upatikanaji wa umeme katika manispaa ya Songea kwani awali kabla ya kuharibika kwa mtambo huo umeme ulikuwa unazalishwa megawati 4.6 kwa mashine zote tano.
"Hata hivyo naomba niwaweke wazi kuwa tatizo hili hatawahusu wale wote ambao wapo katika maeneo muhimu kama vile hospitali na baadhi ya maeneo ya makambi ya jeshi na mjini kati kutokana na unyeti wa shughuli zake.
Aidha alisema kuwa hawezi kusema kuwa tatizo hilo litakwisha lini kwani mafundi wako kazini  wakiwa wanafanyia matengenezo mtambo huo ambao ndio tegemeo kubwa kwa kufua umeme katika halmashauri ya manispaa ya Songea na vitongoji vyake.
Hata hivyo baadhi ya waandishi wa habari walimtaka meneja huyo wa Tanesco Mhandisi Kebara ahakikishe kuwa anakuwa makini katika kuwasimamia mafundi waliofika kufanyia matengenezo matambo huo na wamemtaka awe makini katika kuhakikisha kuwa wananchi wa manispaa hiyo wanapata umeme wa mgao bila kuwepo a upendeleo wa baadhi ya mameneo.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top