Loading...

WAHAMIAJI HARAM 16 RAIA WA ETHIOPIA WAHUKUMIWA JELA MIEZI 12 KILA MMOJA BAADA YA KUSHINDWA KULIPA FAINI YA SHILINGI 50000 KWA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI

MAHAKAMA ya hakimu mkazi Mkoa wa Ruvuma imewahukumu raia kumi na sita wa Nchi ya Ethiopia kulipa faini  ya Sh. 50,000 kila mmoja au kwenda jela mwaka mmoja kila mmoja baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kuingia nchini bila ya kuwa na vibali ambapo wameshindwa kulipa faini na wamepelekwa gerezani kuanza kutumikia kifungo cha miezi kumi na mbili.

Hakimu mkazi wa  mahakama hiyo Casmili Mwarunyungu akisoma hukumu hiyo alisema kuwa washtakiwa kwa vile wamekiri wenyewe kosa mahakamani hivyo mahakama inawapa adhabu ya kulipa faini  ya sh.50,000 au kwenda jela mwaka mmoja kila mmoja .
Kwa upande wake mwendesha mashtaka toka ofisi ya idara ya uhamiaji Greta Banda alidai mahakamani hapo kuwa Yeremias Aremu na wenzake kumi na tano ambao ni raia wa Nchi ya Ethiopia inadaiwa Januari 25 mwaka huu majira ya saa 4 usiku huko katika eneo la kijiji cha Mtyangimbole kwa pamoja walikamatwa na askari wa polisi ambao warishirikiana na maafisa uhamiaji bila kuwa na vibali vinavyowaruhusu kuwepo katika Nchi ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kwa mara ya kwanza walifikishwa mahakamani Januari 29 mwaka huu ambapo mwendesha mashtaka toka Idara ya Uhamiaji Greta Banda aliiomba mahakama hiyo kuhairisha kesi hiyo kutokana na kutokuwepo mkalimani wa kutafsiri lugha ya ARMARIC ambayo ndio inayotumika Nchini Ethiopiakwa kutafsiri katika lugha ya Kiswahili.

Alieleza zaidi mahakamani hapo kuwa mtaalam wa kutafsiri lugha hiyo alikuwa ameandaliwa kufika mahakamani Januari 30 mwaka huu toka shule ya sekondari ya De Poul l iliyopo katika manispaa ya Songea hivyo mahakama ilikubali ombi la mwendesha mashtaka kisha kesi hiyo iliahirishwa na kuletwa tena mahakamani jana (leo).

Washttakiwa wote kwa pamoja baada ya kusomewa shitaka lao warikili kosa na kukubaliana na maelezo ya shitaka yaliyosomwa na mwendesha mashtaka toka idara ya uhamiaji Banda hivyo mahakama iliwatia hatiani kama walivyoshitakiwa na kuwahamuru walipe faini y ash. 50,000 kila mmoja au kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela kila mmoja na wote wameshindwa kutimiza sharti la kulipa faini.




Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top