Loading...

ASKARI POLISI ALIYEJERUHIWA MKOANI RUVUMA KATIKA MAUAJI YA WATU WAWILI APELEKWA MUHIMBILI KWA MATATIBABU ZAIDI


ASKARI Polisi,Venance Kamugisha aliyejeruhiwa  katika vurugu zilizosababisha vifo vya mwananchi mmoja na Askari Polisi  PC Yohana  anasafirishwa kwa ndege  kupata  matibabu zaidi katika Hospitali ya  taifa Muhimbili Jijini Daressalaam .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Deusdedit Nsimeki amewaambia waandishi wa habari kuwa majeruhi huyo  alisafirishwa jana jioni kwa ndege ya abiria  kwenda  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kufanyiwa vipimo zaidi.

Alisema kuwa hali ya Askari huyo inaendelea vizuri ambapo juzi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu alimtembelea Askari huyo katika Hospitali ya Mkoa  huo  kumjulia hali majeruhi huyo wa tukio ambalo limezua mjadala mkubwa katika mkoa wa Ruvuma na Nchini kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mko huo Dkt Philis Nyimbi anasema kuwa wamefanikiwa kumtibu mgonjwa huyo na  hali yake inaendelea vizuri na kwamba  baadhi ya vipimo alivyofanyiwa uchunguzi vimeonesha kuwa hana tatizo.

‘Lakini kutokana na majeraha ya kichwani imelazimika apelekwe Hospitali ya Taifa  Muhimbili katika kitengo cha mifupa kwa ajili ya kufanyiwa vipimo zaidi ambavyo katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma hatuna’alisema  Daktari huyo.

Alibainisha kuwa katika Hospitali hiyo hawana kipimo cha Computer Temography(TC SCAN) ambacho kinatumika kuangalia ubongo na ndicho ambacho Askari huyo anatakiwa akafanyiwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Daressalaam.

Machi 23 mwaka huu katika kijiji cha Ngwinde Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma Askari Polisi PC Yohana mwenye namba 7771 aliuawa na wananchi  waliochukizwa na Askari huyo kumfyatulia risasi mwendesha Pikipiki na kumuua.

Wananchi  hao walimuua askari huyo kwa mawe na kumjeruhi PC Kamugisha ambaye alijeruhiwa baada ya kupigwa kwa mawe wakati wakimuua Askari mwenzake PC  Yohana ambaye mwili wake umesafirishwa kwenda wilayani Kibondo Mkoani Kigoma kwa mazishi.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top