Loading...

MBARONI KWA KUKUTWA AKIFANYA MAPENZI NA MBUZI SONGEA

Picha haihusiani na tukio

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limemtia mbabroni Rajabu Mbunda(30) mkazi wa kijiji cha Mkumbi wilaya ya Mbinga kwa tuhuma za kukutwa akiwa ndani ya banda la Mbuzi huku akifanya mapenzi na Mbuzi jike.

Akizungumza  Ofisini kwake kamaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Revocatus Malimi alisema kuwa tukio hilo limetokea januari 18 mwaka huu majira ya saa sita na nusu usiku huko katika kijiji cha Mipeta kilichopo kata ya Mhukulu wilayani songea.

Kamanda Malimi alisema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio Mbunda alikutwa akiwa ndani ya banda la mbuzi  linalomilikiwa na Twaini Mbele(45) mkazi wa kijiji hicho.

Alifafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo hiyo kabla ya tukio mtuhumiwa mbunda aliku amekwenda kwenye nyumba hiyo kwa ajili ya kunywa pombe kwa kuwa kwenye nyumba hiyo kuna klabu cha pombe za kienyeji ambapo alipomaliza kunywa aliaga kuwa anaondoka  na kuacha watu wengine wakiendelea kunywa pombe akiwemo na mmiliki wa nyumba hiyo ambaye alikuwa anaendelea kuwauzia kinywaji.

Alifafanua zaidi zaidi  kuwa inadaiwa mtuhumiwa Mbunda baada ya kuondoka kwenye kilabu  hicho alielekea kwenye banda la mbuzi ambako baadaye alikutwa na mpita njia huku akifanya mapenzi na mbuzi.

Alieleza zaidi kuwa mpita njia huyo ambaye jina lake limehifadhiwa wakati akipita kwenye eneo hilo la tukio alisikia mbuzi wakipiga kelele na alipowamulika tochi alimuona mbunda akiwa ndani ya banda hilo huku akiwa amemshika mbuzi akiendelea kufanya mapenzi alikimbia hadi kwenye kilabu na kuwaarifu watu waliokuwepo baadaye walilazimika kuongozana naye kwenda na kumkuta mbunda akiendelea kufanya mapenzi na huyo mbuzi.

Alisema kuwa baadaye watu waliokuwa kwenye eneo hilo la tukio akiwepo na mmiliki wa mbuzi huyo walifanikiwa kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji hicho na kumfungia na baadaye walimpeleka kituo cha polisi kwenye kijiji cha Magagula ambao walika na kumchukua na kumpeleka mahabusu.

Alisema uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa mtuhumiwa Mbunda ni mkazi wa kijiji cha Mkumbi wilayani Mbinga ambaye inadaiwa alikuwa amekwenda kwenye kijiji hicho oktoba mwaka jana kwa lengo la kutafuta vibarua vya kulima na kwamba muda wowote kuanzia sasa mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi wa tukio kukamilika.
Na Gideon Mwakanosya –Songeayetu.blogspot.com



1 comments:

Mungu wangu sasa tunakokwenda sijui ni wapi? inasikitisha sana sana hili Tukio kwa kweli

Reply

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top