Loading...

WANANCHI WAHAMASISHWA KULIPIA GHARAMA ZA UPIMAJI WA VIWANJA

Na Stephano Mango, Songea

WANANCHI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma ambao wamepiwa ardhi yao katika Kata ya Mshangano kwa kutumia Kampuni ya Ardhi Plan wametakiwa kulipia gharama za upimaji ili wananchi wengine waweze kuonyeshwa na kuuziwa maeneo haya kwa kuyaendeleza

Wito huo umetolewa jana na Diwani wa Kata ya Mshangano Faustini Mhagama wakati akiwahutubia mamia ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kata hiyo na kuhudhuriwa na Viongozi wa Kampuni ya Ardhi Plan yenye makao makuu Jijini Dar Es Salaam

Mhagama alisema kuwa Mradi ulioibuliwa na wananchi wa Kata hiyo wa kurasimishiwa ardhi yao umekamilika ambapo jumla ya viwanja elfu 18,000 vimepiwa kwa kutumia kampuni ambavyo wananchi wanapaswa kuvilipia haraka ili viweze kugawiwa Septemba 3 mwaka huu kama makubaliano ya awali wakati wa mradi unaanza mwaka 2011 yalivyofikiwa

Alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawapa fursa wananchi kuweza kuishi kwenye maeneo yaliyopimwa, pia watatumia maeneo hayo kwa kupata mkopo na kuendesha miradi mbalimbali ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto
Alisema kuwa ili wananchi waweze kuonyeshwa na kupewa maeneo yao rasmi na kuonyeshwa mipaka ya maeneo yenye shughuli za kijamii wanapaswa kulipia gharama za upimaji zilizokubaliwa kwenye mikutano ya hadhara wakati wa mradi unaanza

Akisoma makubariano yaliyofikiwa wakati wa mradi unaanza mwaka 2011 kwenye mkutano huo Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mshangano alisema kuwa gharama za mradi huo zinatolewa na wananchi wenyewe kwa kutoa ardhi badala ya kusubiri Serikali mpaka ipate uwezo wa kifedha ambapo kwa wale wenye maeneo madogo yaani kiwanja kimoja mpaka viwili wanatozwa gharama ya fedha shilingi laki moja(100,000/=) kwa kiwanja kimoja na laki mbili(200,000) kwa viwanja viwili kama gharama za upimaji


Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top