Loading...

maandamano ya waandishi wa habari songea yaota mbawa

(PICHA NA STEPHANO MANGO) KATIBU WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA RUVUMA( RUVUMA PRESS CLUB) AMBAYE PIA NA KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA SONGEA MJINI DKT EMMANUEL NCHIMBI) ANDREW CHATWANGA

Na Gideon Mwakanosya

MGOGORO mkubwa umeibika kwa waandishi wa habari mkoani Ruvuma baada ya Viongozi wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo kutoitisha maandamano na kuingia mafichoni kwa muda ili kuepusha kufanyika maandamano ya kuunga mkono maombolezo ya kifo cha mwandishi wa habari na aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa Daud Mwangosi aliyefariki kwa kupigwa na mlipuko uliosababishwa na polisi katika kijiji cha Nyololo mkoani Iringa.

Mgogoro huo umewagawa waandishi wa habari na kuwafanya baadhi ya waandishi kutishia kujitoa nafasi zao za uongozi na uanachama.

Waandishi wa habari mkoani Ruvuma walianza kwa walishangazwa na hatua ya viongozi wa ngazi ya juu ya chama hicho kutowajulisha muda na njia zitakazotumika kwa maandamano hayo hadi pale kwa njia ya simu na baadhi ya waandishi wa habari ambao walishapanga waandamane saa 10. Jioni baada ya kujihakikishia kuwa viongozi wao wamewatosa nan hawana ajenda muhimu ya kupinga m,aandamano hayo kwa hula.

Awali baadhi ya waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali ambao ni wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo (RPC) walijikusanya pamoja na kufuatilia matangazo ya vyombo mbali mbali vya habari yaliyokuwa yakiendelea huku wakiangalia baadhi ya picha zilizopigwa wakati na baada ya kifo cha mwandishi huyo wa habari ambaye alipatwa na mauti wakati akiwa kazini na walipanga wandamane saa 10 jioni muda ambao ndio Marehemu Mwangosi aliuuawa kinyama kupigwa na bomu na Polisi.

Katibu Msaidizi was Chama cha wqaandishi wa habari Mkoa wa Ruvuma , Julius Konala, alionyesha ushirikiano mkubwa kwa wanachama ambao muda wote walikuwa wanadai rauba na hatua iliyofikiwa na viongozi wa chama hicho kwaqajili yua maandamano na kuwajulisha kuwa viongozi wake hawajulikani waliko na wanapinga kufanyika kwa mnaandamano hayo.

“Jamani mimi mtanionea tuu, Mwenyekiti na katubu wamesema kuwa UTPC imeyasimamisha maandamano yetu bila kutaja sababu,” alisema Konala ambaye alichukua hatua ya kuwasiliana na viongozi wa polisi mkoani hapa waliotaka kujua ni njia zipi zitakazotumiak katiak maandamano hayo ili walete askari waq kuyalinda maandamano hayo ya amani.

Tukio hilo limewakasirisha sana viongozi wa Chama hicho na kulazimika kuitisha mkutano wa dharura kwa baadshi ya wanachjama wengi wao wakiwa ni mamluki na kusababisha viongozi hao kuomba radhi kwamba wamekosa mawasiliano nao na baadhi ya wanachama wametushia kujiuzulu akuwemo katibu msaidizi Julius Konala kwa madai kwamba chama hicho kimeingiliwa na mikono ya wanasiasa.
“naona mbele yangu kuna wingu kubwa ambalo mwisho wake siujui, nafikiria kujiuzulu uongozi na kujitoa kataika chama, “ alisema Konala.

Baadhi ya wadau wa habari mkoani humo wamenesha kushangazwa na ukimya wa wanahabari wa mkoa huo liocha ya wanahabari wote nchini wakionekasna kwenye runinga wakiandamana kupinga ukatili huo iliofanywa dhidi ya Mwandishi wa habari akiwa kazini.

Hata hivyo Mkurugenzi wa muungano wa Vyama vya waandishi wa habari nchini UTPC Abubakar Karsan akiongea na Nipashe kwa njia ya Simu amekanusha vikali kwamba wao walitoa maelekezo kwa Ruvuma Press Club kwamba wasiandamane kwa madai kuwa viongozi hao waliwajulisha kuwa maandamano hayo yatatekwa na CHADEMA.


Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top