Loading...

Diwani ashikiliwa na Polisi kwa kuwapiga wauguzi wa kituo cha afya

JESHI  la  polisi  mkoani Ruvuma  linawashikilia watu wawili  akiwemo  Diwani wa kata ya Ruchiri (CCM ) Wilaya  ya  Namtumbo kwa tuhuma za  kuwapiga  wauguzi wawili  wa zahanati  ya kanisa katoriki  jimbo kuu la songea parokia  ya Namtumbo kigango  cha  Chengena sehemu mbalimbali  za mwili kwa mawe, fimbo na mateke na  kumsababishia muuguzi mmoja kati yao kulazwa katika hospitali ya  serikali ya  mkoa.
 
Akizungumza na NIPASHE  jana mchana ofisini kwake kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma  Mrakibu  mwandamizi wa polisi  George Chiposi  aliwataja watuhumiwa  kuwa ni  Zacharia  Mapunda  maarufu kwa jina la chepa (46) ambaye ni diwani wa kata ya Ruchiri  na mtoto wake  Andrew  Mapunda  (24) mkazi wa kijiji cha Chengena.
 
Aliwataja wauguzi  waliojeruhiwa kwa kupigwa  ni  Emmacurata Komba (29) na Rose  komba  (35)  ambao wote ni wauguzi wa zahanati wa kanisa katoliki jimbo kuu la songea parokia  ya Namtumbo kigango cha Chengena.
 
Kaimu kamanda Chiposi  alisema  kuwa tukio hilo lilitokea  januari 13 mwaka huu  majira ya saa  5 asubuhi huko katika kijiji cha Chengena  ambako inadaiwa  Emmacurata  na Rose walipigwa na  Diwani  wa kata ya Ruchiri ambaye alishilikiana na mtoto wake  Andrew.
 
Alifafanua zaidi kuwa  inadaiwa kiini cha ugomvi kuwa  ni kwamba  awali  Emmacurata alikuwa ni mpangaji wa nyumba inayomilikiwa na mapunda maarufu kwa jina la Chepa ambaye ni diwani wa kata hiyo na  kutokana na juhudi zake nyumba hiyo aliikarabati  kwa kuisakafia  na kuweka milango pamoja na madirisha mapya.
 
Alibainisha zaidi kuwa  pamoja na jitihada hizo alizozifanya Emmacurata inadaiwa watoto wa diwani  hawakutaka mpangaji huyo aendelee kuishi kwenye nyumba  ya baba yao kwa madai kuwa kwa muda mrefu alikuwa halipi kodi ya pango la nyumba.
 
Alisema  kutokana na  mvutano huo  Emmacurata alifikia  huamuzi wa kuama nyumba hiyo na kwenda kuamia nyumba nyingine ambayo ilikuwa bado haijakamilika kwa kutokuwa na madirisha na milango hivyo aliamua kwenda  kwenye nyumba aliyokuwa akiishi awali  kungoa  madirisha na milango ili akaweke kwenye nyumba nyingine ambayo alitarajiya  kuamia ndipo ugomvi ulianza  kwa diwani wa kata hiyo Mapunda  kwa kushilikiana na mtoto wake Andrew  walimpiga Emmacurata kwa mawe, mateke na ngumi sehemu mbalimbali za mwili.
 
Kaimu kamanda Chiposi  alifafanua zaidi kuwa  wakati ugomvi huo ukiendelea  ghafla Rose alifika kwenye eneo la tukio  na alikwenda  kuamua ugomvi naye alipigwa jiwe kichwani ambaye  alipelekwa kwenye hospitali ya serikali ya Wilaya ya namtumbo ambako alitibiwa na kuruhusiwa  kurudi nyumbani.
 
Alisema  baadae hali yake ilibadilika ghafla  kuwa mbaya kisha alikimbizwa katika hospitali ya serikali ya mkoa  ambako amelazwa anaendelea kupata matibabu katika wodi   grade  namba 2.
 
Alisema polisi inafanya upelelezi kuhusiana na tukio hio  na kwamba utakapokamilika  watuhumiwa wanatarajiwa kufikisha mahakamani kujibu mashitaka yanayo wakabili.
 
Hata hivyo  mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa  Dr. Benedicto Ngaiza  alipohojiwa na NIPASHE  kwa njia simu kuhusiana na majeruhi  wa tukio hilo  alisema kuwa Rose Komba  aliletwa hospitalini hapo januari 13 mwaka huu majira ya saa za usiku akiwa na hali mbaya lakini  kwa hivi sasa anaendelea vizuri licha ya kuwa bado hajaruhusiwa kurudi nyumbani.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top