Loading...

Watu watatu wapigwa radi Namtumbo





WATU watatu wa familia moja wakazi wa kijiji cha Winga kilichopo katika Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamejeruhiwa vibaya kwa kupigwa a radi njee ya nyumba yao wakati wanakula chakula cha mchana baada ya kutoka kwenye shughuli zao za shamba.
Kaimu kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Mrakibu mwandamizi wa Polisi  Gorge Chiposi  amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Zainabu Ally (33),Ally Khamisi (5) na Hawa Nigange (4)wote wakazi wa kijiji cha Rwinga nje kidogo ya mji wa Namtumbo.
Kaimu kamanda Chiposi alisema tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 11 jioni huko katika kijiji cha Rwinga ambako watu watatu wa familia moja wakiwa wanakula chakula nje ya nyumba yao ghafla mvua ya upepoe ambayo iliambatana na radi ilianza kunyesha na baadae wakiwa wanaendele kula chakula walipigwa na radi na kuwasababishia majeraha sehemu mbalimbali ya mihili yao.
Alifafanua kuwa inadaiwa Zainabu ambaye ni mama mzazi wa watoto hao alipigwa na radi na kusababisha miguu yote miwili kupooza ,Mtoto Ally radi ilimbabua maeneo ya paja la kushoto,tumboni na kwenye makalio yake na mtoto Hawa alibabuliwa na radi mikononi na tumboni.
Alisema kuwa majeruhi wote walikimbizwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya ya Namtumbo ambako wanaendelea kupata matibabu na hali zao bado sio nzuri hata hivyo mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali mkoani humo zimeharibu miundombinu ya barabara na kusababisha usafiri kuwa mgumu.
Baadhi ya wakazi wa manispaa ya Songea wamejikuta wakikosa huduma za mitandao ya E-mail (barua pepe ) ambayo imesababisha huduma za ATM za taasisis za kifedha zilizopo mkoani humo na barua pepe kutofanya kazi tangu Juzi kufuatia mvua kubwa iliyonyesha ikiambatana na radi kuharibu miundombinu ya mawasilia



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top