Loading...

Mwendesha Boda boda akutwa na polisi akiwa na risasi mjini Songea



MWENDESHA pikipiki Dastan Mbena (30) mkazi wa Songea mjini anashikiliwa na polisi mkoani Ruvuma akikabiliwa na tuhuma za kukutwa na risasi saba zinazodaiwa kuwa ni za bunduki aina ya Riffle ambazo alikuwa amezibeba kwenye mfuko uliofungwa nyuma ya pikipiki aliyokuwa akiendesha akitokea katika kijiji chA Namabengo wilayani Namtumbo kwenda Songea mjini.

Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma mrakibu mwandamizi wa polisi George Chiposi alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa nne asubuhi huko katika kijiji cha Mtwara pachani kulichopo katika wilaya ya Namtumbo wakati akitokea namabengo kwenda Songea mjini.

Kaimu kamanda Chiposi alifafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio askari polisi ambao walikuwa kwenye doria kwa kazi maalum ambao waliongozwa na mkaguzi msaidizi wa polisi Adam Kimbesi walimkamata Mbena baada ya kumkimbiza kwa muda mrefu akiwa kwenye pikipiki yenye namba za usajili T536 BGX aina ya SanLg aliyokuwa akiiendesha.

Alisema kuwa askari hao baada ya kufanikiwa kumkamata walimpekua na kukuta kwenye mfuko uliokuwa umefungwa nyuma ya pikipiki hiyo ndani yake kulikuwa na risasi saba zinazotumika kwenye bunduki aina ya riffle.

Hata hivyo kaimu kamanda chiposi alisema kuwa mtuhumiwa amekamatwa na anatrajiwa kufikishwa mahakamani pindi upelelezi wa tukio hilo utakapo kamilika.




Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top