Loading...

UKUTA WAANGUKIA MAGARI, WAJERUHI WATATU KITUO CHA MABASI UBUNGO

 

 
Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.
Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.
Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.
Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.
Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.
Ilikuwa ni hasara tupu.
Hali ilikuwa ni mbaya katika zahama hiyo ya alfajiri ya leo.
Watu wakiangalia magari yao.
‘Noah’ hili halikuepuka janga hilo.
Kenyela akiongea jambo juu ya ajali hiyo.
Mkatisha ushuru wa maegesho hayo akiendelea kukusanya ushuru.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo.
SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo alfajiri umeanguka na kuyaharibu vibaya magari zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa nje ya eneo hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL
 



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top