Loading...

Ajali ya gari yasababisha kifo mkoani Ruvuma


JESHI la polisi mkoani Ruvuma limemtia mbaroni Barnabas Chipeta (25) mkazi wa mahenge katika halmashauri ya manispaa ya Songea kwa tuhuma za kusababisha kifo cha aliyekuwa  abiria wake kwenye gari aliyokuwa akiiendesha kutoka Songea kwenda Mbinga ambayo ikiwa kwenye mwendo mkali iliacha njia na kupinduka.

Akizungumza ofisini kwake kaimu kamanda wa polisi mrakibu mwandamizi wa polisi George Chiposi  alisema kuwa tukio hio lilitokea juzi majira ya saa tatu usiku huko katika kijiji cha Liganga wilaya ya Songea vijijini.

Kaimu kamanda Chiposi alibainisha zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio kwenye barabara itokayo Songea kwenda Mbinga  gari lenye namba za usajili T104 ANM aina ya Mitsubishi Canter iliyokuwa ikiendeshwa na Chipeta ikiwa kwenye mwendo mkali ikitokea Songea kwenda Mbinga iliacha njia na kupinduka na kusababisha kifo cha Iddi Said(25) mkazi wa madizini manispaa ya Songea.

Alisema kuwa dereva Chipeta akiwa na abiria huku akitambua kuwa anavunja sheria aliendesha gari kwa mwendo kasi ambaoulimsababishia ashindwe kabisa kuumudu usukani jambo ambalo lilimfanya apate ajali hiyo ambapo abiria wake Iddi Said alifariki papo hapo.

Alieleza kuwa chanzo ni mwendo kasi ambao pia ulisababisha magurudumu ya mbele ya gari hiyo kupasuka baada ya kutokea ajali na kwamba dereva wa gari hiyo wakati anafanya jitihada za kutaka kukimbia wananchi wa kijiji hicho walimkamata na kwa sasa yupo mikononi mwa polisi na upelelezi zaidi wa tukio hilo unafanywa na utakapokamiliza atafikishwa mahakamani kujibu shitaka hilo.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top