Loading...

Sifa za Watakaochaguliwa kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba zatajwa

                                     Wajumbe wa kuandaa rasimu ya katiba mpya Tanzania

Sifa za Watakaochaguliwa kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya, Ngazi ya Serikali za Mitaa

Wajumbe wanne kutoka kila Kata kwa Tanzania Bara na wanane kutoka kila Kata katika Mkoa wa Dar es Salaam na Wajumbe watatu kutoka kila Shehia kwa Zanzibar wanapaswa kuwa na sifa zifuatazo:
1.1.Awe Raia wa Tanzania.
1.2.Awe na umri wa miaka 18 au zaidi.
1.3.Awe na uwezo wa kusoma na kuandika.
1.4.Awe mkazi wa kudumu wa Kijiji/ Mtaa / Shehia husika.
1.5.Awe Mtu mwenye hekima, busara na uadilifu.
1.6.Awe Mtu mwenye uwezo wa kujieleza na kupambanua mambo.

MAMBO YA KUZINGATIWA
Utaratibu wa kuwapata Wajumbe kwa Tanzania Bara na Zanzibar uzingatie mambo yafuatayo:-
2.1.Uwakilishi wa watu wazima.
2.2.Uwakilishi wa wanawake.
2.3.Uwakilishi wa vijana.
2.4.Jiografia ya Kata/ Wadi / Kijiji / Mtaa / Shehia husika



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top