Loading...

Mradi wa Albino waanzishwa kanda ya ziwa

Mmoja wa mlemavu wa ngozi (Albino) aliketwa mikono na watu wenye imani ya kishirikinaNa Sophia Kingimali
SHIRIKA inayoshughulikia walemavu wa ngozi Under the same sun (UTSS) ikishirikiana na Serikikali ya Canada kupitia ubalozi wake nchini Tanzania imeanzisha mradi wa redio katika kanda ziwa.
Mradi huo umezinduliwa leo jijini Dar es salaam na hafisa mradi bi Rachel Moyoikiwa na lengo la kuelimisha jamii na kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu albinism.
Aidha Moyo amesema kuwa watatumia redio za kijamii zilizopo kanda ya ziwa kuendesha vipindi katika mtindo wa makala mchanganyiko,majadiliano ya moja kwa moja pamoja na mchango wa simu kutoka kwa wasikilizaji na pia michezo ya kuigiza.
"Jopo la majadiliano la moja kwa moja ambalo litaendeshwa ni pamoja na mazungumzo kati ya watu wenye albinism na wataalamu wa maswala ya albinism ikiwa ni pamoja na michango ya wasikilizaji kwa njia ya simu" alisema Moyo.
Moyo ameongeza kuwa redio zitakazoendesha vipindi vya “tambua albinism”ni pamoja na Sengerema Fm,Sibuka Fm,Faraja Fm,Fadeco Fm,Kahama Fm na Chemchem Fm pia ametoa wito kwa redio ambayo itakayo kuwa tayari kushiriana nao wataipa ushirikiano.

via: http://www.habarimpya.com


Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top