Loading...

SUMATRA YATANGAZA VIWANGO VIPYA VYA NAULI ZA MABASI NCHINI

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini SUMATRA imetangaza viwango vipya vya nauli za mabasi ya masafa marefu, daladala katika jiji la Dar es Salaam, nauli za usafiri wa reli ya kati na bandari.

Viwango hivyo vimetolewa kutokana na SUMATRA kufuatia maombi rasmi kutoka kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri na makampuni binafsi nchini kutokana ongezeko la gharama za uendeshaji.
Ahmad Kilima ni Kaimu mkurugenzi mkuu wa SUMATRA amesema viwango vipya vimetolewa baada ya kufuata taratibu za kisheria na utendaji kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali katika kujadili na kupata maoni yao kuhusu ongezeko la nauli.

Amesema SUMATRA imeongeza viwango vya juu vya nauli ya daladala kwa wastani wa asilimia 24.46 na mabasi ya masafa marefu viwango vimeongezwa kwa asilimia 20.3
Pia amesema ili kuhakikisha kuwa kuna uwiano kati ya viwango vipya vya nauli na ubora wa huduma ya usafiri, mamlaka imewataka wamiliki wa mabasi kutotumia wapiga debe katika kuuza tiketi za usafiri na kwamba watakaokaidi hatua za kisheria zitachukuliwa.

Bwana Kilima amesema katika kufanya mapitio ya gharama mbalimbali za bandari na bahari kuu mamlaka imeridhia ongezeko la gharama kwa wastani wa asilimia 34.3 hivyo TPA wametakiwa kuboresha huduma kwa wateja kwa kuanzisha kitengo cha huduma kwa wateja .

Hata hivyo ongezeko hilo la nauli limeenda sanjari na viwango vya nauli kwa usafiri wa abiria wa reli ya kati ambapo mamlaka imewataka abiria kukata tiketi na kupanda treni wakionyesha vitambulisho…

Viwango vipya vya nauli vinatarajia kuanza kutumika kuanzia tarehe 12 Aprili 2013 ambapo nauli ya mwanafunzi itakuwa shilingi 200 na mtu mzima atalipa shilingi 400 kwa safari za mijini.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top