Loading...

Zitto awawashia Moto TANESCO Songea na Kutoa Onyo Kali kwa IGP na RPC



Na songeayetu.blogspot.com
 
Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demakrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za mashirika ya umma, mheshimiwa  Zitto Kabwe amewahakishia wakazi wa manispaa ya Songea kumaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa nishati ya umeme ambayo kwasasa limekuwa kero kubwa wa wananchi wa manispaa hiyo kwakuwa lipo ndani ya uwezo wake.

Zitto aliyasema hayo jana jioni wakati  akihutubia maelfu ya wapiga kura katika kata ya Lizaboni iliyopo ndani ya manisapaa ya Songea.Wananchi wa kata ya Lizaboni wanataraji kufanya uchaguzi mdogo ili kumpata diwani ambaye ataziba pengo la aliyekuwa diwani wa kata hiyo marehemu Manya.

Katika hotuba yake mheshimiwa Zitto amewahakikishia wakazi wa Songea kuwa atahakikisha wafanyakazi wa TANESCO ambao wamekuwa na tabia ya kuiba mafuta ya jenereta za kuzalishia umeme wanachukuliwa hatua za kisheria haraka iwezekanavyo ili kuondoa tatizo la umeme linaloukabili mji wa Songea na viunga vyake. 

Zitto alisema akiwa mwenyekiti hesabu za mashirika ya umma atashughulikia tatizo hilo kwa kufanya mambo mawili kwanza kwa kuwahoji kwanini umeme ukatike hovyo Songea? Pili matumizi ya mafuta yanatumikaje?  Kisha baada ya hapo mtiti wake mtauona. Alisema kama ameweza kumshughulikia mkurugenzi wa TANESCO Tanzania, kwa Songea itakuwa ni kitu kidogo kwake.

 Katika kuondoa kabisa tatizo la umeme katika mkoa wa Ruvuma alisema ujenzi wa mitambo mikubwa ya kuzalisha umeme kwa makaa ya mawe inajengwa  Mbinga yenye uwezo wakuzalisha megawati 120 na mji wa Songea utapata kilovoti 220 pia katika kufanya tatizo hili kuwa ndoto kabisa, mkoa wa Ruvuma utaunganishwa na gridi ya taifa kutoka Makambako mkoani Njombe.

Aidha, Zitto Kabwe alitoa onyo kali kwa IGP na RPC wa mkoa wa Ruvuma endapo wataendelea na mpango wao wa kutaka kumletea zengwe mgombea wa udiwani wa kata ya lizaboni kuwa anatuhuma zinazomkabili toka mwaka 1988, CHADEMA wameinasa barua waliyoandikiana wakuu hao wa jeshi la polisi. Zitto amehoji iweje tuhuma hizo zifumbiwe macho toka mwaka 1988 walikuwa wapi wakati mgombea huyo alivyokuwa kiongozi wa mtaa kwa vipindi viwili? Pia inasemekana katika barua hiyo diwani huyo anaundiwa zengwe linaloonesha kuwa yeye alikuwa anachochea waendesha pikipiki waandamane na kuleta fujo katika kipindi cha mauaji yaliyokea miezi michache iliyopita mjini hapa. Zitto amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina wa mauaji yaliyotokea na si kutishia raia. Katika kukomesha kabisa tabia hiyo inayotaka kufanywa na polisi Zitto ameahidi kuipeleka barua hiyo bungeni. 

Pia alisema kuna tetesi za jeshi la polisi kuwa na mpango wa kuleta polisi wengine kutoka nje ya mkoa wa Ruvuma siku ya uchanguzi ili kuwadhibiti wananchi wa Lizaboni washindwe kupiga kura siku ya uchaguzi kwakuwa sasa polisi wa Songea wengi wanakinga mkono chama hicho.


Wanachama na wafuasi wa CHADEMA wakiandamana



Waendesha pikipiki wakiwa katika maandamano


Mamia ya Wananchi wakiwasili katika mkutano wa CHADEMA

Mh. Zitto Kabwe akiwasili katika viwanja vya mkutano

Mh. Zitto Kabwe na Mh. Chiku Abwao

Mh. Zitto na Mgombea udiwani

Makamu mwenyekiti BAVICHA akimwaga sera Songea

Mh. Zitto akiunguruma jukwaani

Mwanachama wa CCM akirudisha kadi ya CCM na kujiunga na CHADEMA



Hata bibi nae alihama CCM na kujiunga na CHADEMA

Balozi wa Mtaa kwa tiketi ya CCM nae ahamia CHADEMA

Piga Kiberiti vikorokoro vya CCM





Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top