Loading...

Ajifungua mtoto, amnyonga na kumzika mjini Songea


Jenista Mapunda (24) mkazi wa Mfaranyaki mjini Songea amejifungua mtoto kisha kumnyonga na kumzika yeye mwenyewe alfajiri na kuweka msalaba wa mti kama ilivyo desturi kwenye maziko.

Jenista alidai kuwa ni kutokana na ugumu wa maisha ndiko kumesababisha alipojifungua karibu na vyoo vya shule ya msingi Misufini kuamua kumnyonga mtoto wake hadi kufa kisha kumbeba na kwenda kuchimba kaburi na kumzika.

Jenista ambaye aliishiwa nguvu kutokana na kutokwa na damu nyingi amekamatwa na polisi ila amepelekwa kupatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma .



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top