Loading...

WANAFUNZI IFM WAANDAMANA,KOVA AWATULIZA

Jeshi la polisi kanda Maalum Dar es Salaam limewataka wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kutulia wakati madai yao ya kuhitaji ulinzi wao na mali zao kufuatia matukio ya kuporwa,kupigwa,kulawitiwa na kubakwa.

Hata hivyo kamanda wa kanda Maalum Dar es Salaam Suleimani Kova amesema atayashughulikiwa madai hayo baada aya kuzungumza na wanafunzi na wananchi wa kigamboni mazungumzo yaliyofanyika katika uwanja wa Machava Kigamboni.
MATUKIO KATIKA PICHA YA MAANDAMANO YA WANAFUNZI IFM JIJINI DAR ES SALAAM
 Wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha IFM wakiwa wamejazana kwenye kivuko huku wakigoma kushuka hata baada ya kuamriwa kwamba kiusalama itakuwa vigumu kwao kusafiria kwenda kigamboni.
Hatimaye wanafunzi wa IFM wamekubali kushuka na kupungua ili kuwapisha wengine na kuvuka kwa awamu kuelekea kigamboni
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia akiwaagiza wanafunzi wa chuo cha uongozi wa fedha IFM kuelekea eneo la uwanja wa Machava kwa ajili ya majadiliano lakini wanafunzi hao wakakataa na kuanza kuongea maneno ya kashfa ndipo mabomu ya machozi yakawatawanya wanafunzi hao.
Baada ya mabomu ya machozi wanafunzi wanajisalimisha kwa kunyoosha mikono juu.
Wanafunzi wakiruka kichura huku wengine wakitembelea magoti 

 Wanafunzi wakipakiwa katika gari ya polisi kuelekea kituo cha polisi Kigamboni 
 
Wanafunzi wa IFM wakiwa chini ya ulinzi wa jeshi la Polisi baada ya rabsha za hapa na pale kutulizwa.
Pata shika nguo kuchanika hapa wanaonekana Wanafunzi wa IFM wakigombea wenyewe kuingia kwenye gari dogo la Polisi kuelekea kituo cha Polisi Kigamboni.
Mwanafunzi wa kike ambaye jina lake halikupatikana mara moja akiwa ameanguka kufuatia kashkash baina ya jeshi la polisi na wanafunzi wa IFM
Mwanafunzi mwingine wa kike akisaidiwa kuinuka baada ya kuanguka katika purukushani hizo.
Mwanafunzi akionekana hajiwezi baada ya kukimbia na kuanguka mara kadhaa kwa mshtuko wa bomu.
Mwanafunzi mwingine akiwa hajiwezi akiugulia maumivu baada ya misukosuko ya hapa na pale
Ni kama wanasema Makamanda tumekubali kurudi meza ya mazungumzo,wanafunzi wakielekea kituo cha polisi Kigamboni kwa mazungumzo na maafisa wa jeshi la Polisi.
Hapa mwenye kutembea kwa magoti haya mwenye kusota kichura chura haya ili mradi wafike Kigamboni Police Post
Wanafunzi wa  IFM wakiwa mbele ya Kituo cha Polisi Kigamboni wakipewa maelekezo na hatimaye wakaelekea uwanja wa Machava kwa mazungumzo na jeshi la Polisi.

Kamanda Kova akizungumza na wanchuo wa IFM wakati wa maandamano.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top