Loading...

Tanzania imezidi kupaa viwango vya FIFA

Vijana wa Taifa Stars wakishangilia moja ya mabao yao ya ushindi           Jackson Odoyo,Arusha
KIPIGO cha mabao 3-1 dhidi ya timu ya Taifa ya Morocco kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, imeipaisha timu ya Taifa ya Tanzania, (Taifa Stars) kwa nafasi 3 zaidi.
Kwa muujibu wa viwango vya soka vilivyotolewa jana na Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA vimeipaisha Tanzania kutoka nafasi 119 mwezi uliopita hadi nafasi 116 mwezi huu.
Tanzania ilianza kupanda katika viwango hivyo baada ya kuichapa Cameroon kwa bao 1-0 kwenye uwanja huo huo kabla ya kukutana na Morocco na kuishushia kipigo cha mbwa mwizi.
Mbali na Tanzania kupanda kwa nafasi hizo tatu bado imeshindwa kuikamata Uganda inayoongoza kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki ikiwa kwenye nafasi ya 92 huku Kenya ikiwa kwenye nafasi ya 122.
Namba moja imeendelewa kushikwa na Hispania huku mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika Nigeria ikiendelea kuwa vinara wa Afrika na kushika nafasi ya 30 duniani.



Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright songeayetu.blogspot.com | Designed By JUNGUKUU.US
Back To Top